VENEZUELA-SIASA
Maduro kutawazwa Alhamisi kama rais wa Venezuela
Rais wa Venezuela Nicolas Maduro anatarajiwa kuapishwa Alhamisi wiki hii Januari 10, kuongoza nchi hiyo kwa muhula wa pili, wa miaka sita. Nicolas Maduro alishinda uchaguzi wa urais kwa asilimia 68 ya kura nchini Venezuela
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Maduro mwenye umri wa miaka 56, ataapishwa na Jaji wa Mahakama ya Juu, katika nchi ambayo bunge linadhibitiwa na wapinzani.
Marekani, Umoja wa nchi za Amerika na Umoja wa Ulaya, zimesema hazimtambua Maduro kama kiongozi halali wa nchi hiyo, na wamekuwa wakishinikiza uchaguzi mpya.
Hata hivyo, anaiungwa mkono na Urusi, China na Uturuki.