Trump: Sikueleweka vema kuhusu Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani
Rais wa Marekani Donald Trump ambaye amekuwa akikosolewa vikali, baada ya matamshi yake ya kuitetea Urusi kuwa haikuingilia uchaguzi wa mwaka 2016, amesema hakueleweka vema.
Imechapishwa:
Trump amesema ana imani kubwa na kitengo cha Inteljensia ncnini Marekani ambacho maafisa wake wamekuwa wakisema Urusi iliingilia Uchaguzi huo.
Nina imani kubwa na nawaunga mkono maafisa wetu wa Inteljensia, na nimekuwa nikisema kuwa, hatua ya Urusi haikuwa na atthari yoyote kwa matokeo ya Uchaguzi. Kama nilivyosema, acha nirudie kuwa, nakubaliana na maafisa wa Intejesnia kuwa Urusi iliingia Uchaguzi wa mwaka 2016.
Urusi imekuwa ikisema hakuingilia Uchaguzi huo wakati huu maafisa wa Iteljesnia wa Marekani wakiendelea na uchunguzi.