Pata taarifa kuu
MAREKANI-KOREA KASKAZINI-MAZUNGUMZO-USALAMA

Marekani kukutana kwa mazungumzo na Korea Kaskazini bila masharti

Marekani kupitia Makamu wa rais wa nchi hiyo Mike Pence imesema kuwa iko tayari kwa mazungumzo na Korea Kaskazini bila ya masharti yoyote.

MAkamu wa rais wa Marekani Mike Pence.
MAkamu wa rais wa Marekani Mike Pence. REUTERS/Ammar Awad
Matangazo ya kibiashara

Kwa mujibu wa gazeti la Washington Post, likimnukuu Bw Pence, ikiwa Korea Kaskazini inataka mazungumzo, basi utawala wa Trump utafanya hivyo, na hakutakuepo na masharti.

Awali utawala wa Trump ulisema kuwa hautafanya mazungumzo na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jon-un ikiwa tu yuko tayari kuachana na mpango wa nyuklia.

.Wadadisi wanasema Marekani imebadilisha msimamo wake dhidi ya Korea Kaskazini baada ya kuonekana kuwa haina ushawishi mkubwa wa kuizuia nchi hiyo kuendelea mpango wake wa silaha za nyuklia.

Hivi karibuni Marekani ilitishia kuivamia kijeshi Korea Kaskazini, ikiionya kuwa itasambaratishwa kama haitaki kuachana na mpango wake wa silaha za nyukilia na kufanya majaribio yake ya makombora ya masafa marefu.

Hata hivyo Makamu wa rais wa Marekani amesema akisisitiza kuwa vikwazo vitakuwepo hadi pale Korea Kaskazini itachukua hatua za kumaliza mpango wake wa silaha za nyuklia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.