Trump asema anaweza kusitisha shughuli za serikali kujenga ukuta mpakani na Mexico
Rais wa Marekani Donald Trump amesema atasitisha shughuli za serikali, kama itamlazimu ili kujenga ukuta katika mpaka wa nchi jirani Mexico.
Imechapishwa:
Trump ametoa kauli hii wakati akiwahotubia mkutano wa hadhara jimboni Arizona.
Aidha, amesema ataliomba bunge la Congress kupitisha mswada wa kumpa fedha za kujenga ukuta huo ambao amesema utakuwa mkubwa na wa kupendekeza.
Trump amekuwa akisema hata kabla ya kuchaguliwa kuwa, atajenga ukuta huo kwa lengo la kuwazuia wahamiaji haramu wanaoingia Marekani.
Wakati uo huo, Trump amevilaumu vyombo vya Habari nchini humo kwa kuyapa nafasi makundi yenye mrengo wa kulia, kuzua wasiwasi nchini humo.
Hivi karibuni, kumekuwa na mapigano kati ya watu wenye mirengo tofauti na ya kibaguzi.
Kamati ya Umoja wa Mataifa imesema suala hili linastahili kutafutiwa ufumbuzi wa haraka ili kuepuka mapigano na mauaji zaidi.