Pata taarifa kuu
MAREKANI-KOREA KASKAZINI-USALAMA

Marekani yafanya mazoezi ya kijeshi kama jibu kwa Korea Kaskazini

Marekani imesema kuwa jsehi lake limefanya mazoezi ya kijeshi kama jibu kwa mjaribio ya hivi karibuni ya Korea Kaskazini baada ya kufanikiwa kuufanyia majaribio mtambo wake wa kujikinga dhidi ya makombora.

Kombora la masafa marefu la ICBM linalokwenda bara hadi jingine wakati jeshi la Korea Kaskazini likifanya jaribio lake mjini Pyongyang.
Kombora la masafa marefu la ICBM linalokwenda bara hadi jingine wakati jeshi la Korea Kaskazini likifanya jaribio lake mjini Pyongyang. KCNA via Reuters
Matangazo ya kibiashara

Pia Marekani imesema imerusha ndege zake aina ya B-1 bomber katika rasi ya Korea.

Ndege za Marekani za B-1 bombers pia zilifanya mazoezi katika eneo la rasi ya Korea zikishirikisha ndege za Korea Kusini na Japan.

Kombora lililofyatuliwa na jeshi la Marekani katika anga za habari ya Pacific liliharibiwa na kombora la Thaad.

Mzoezi hayo yanafanyika siku mbili baada ya Korea Kusini kufanya jaribio la pili la kombora la masafa marefu aina ya ICM.

Siku ya Jumamosi rais wa Marekani Donald Trump aliilaumu China kwa kushindwa kuidhibiti Korea Kaskazini katika mipango yake ya nuklia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.