Pata taarifa kuu
MAREKANI-NATO

Trump abadilisha mtazamo wake kuhusu jeshi la NATO

Rais wa Marekani Donald Trump ameonesha kubadilisha msimamo wake kuhusu jeshi la muungano wa nchi za Mataifa ya Magharibi NATO.

Rais wa Marekani Donald Trump akisalimiana na Katibu Mkuu wa NATO  Jens Stoltenberg, katika Ikulu ya White House  Aprili 12 2017
Rais wa Marekani Donald Trump akisalimiana na Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg, katika Ikulu ya White House Aprili 12 2017 REUTERS/Jonathan Ernst
Matangazo ya kibiashara

Trump amesema jeshi hilo ni muhimu sana kutokana na ongezeko la visa vya ugaidi vinavyongezeka katika maeneo mbalimbali duniani na haliwezi kupuuzwa.

Kiongozi huyo wa Marekani aliyekutana na Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg katika Ikulu ya White House, amelitaka jeshi hilo kuzidisha makabiliano dhidi ya makundi ya kigaidi hasa nchini Iraq na Afganistan.

Wakati wa kampeni ya kuwa rais mwaka uliopita, Trump alinukuliwa akisema haoni umuhimu wowote wa jeshi la NATO  huku akisema  Marekani imeendelea kutumia fedha nyingi kulifadhili.

Stoltenberg amesema kuwa mazungumzo yake na rais Trump yalikwenda vizuri na walizungumza mengi kuhusu namna NATO inavyoweza kuisaidia kupambana na ugaidi.

Hata hivyo, Trump ameyataka mataifa yanayochangia katika jeshi hilo kusaidia kuchangia fedha kufanikisha operesheni za NATO.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.