Marekani: Trump na Hillary washinda katika majimbo muhimu
Mgombea kwa tiketi ya chama cha Republican Donald Trump na mgombea kwa tiketi ya chama cha Democratic Hillary Clinton wote wamepata ushindi mkubwa Jumanne hii katika kura za mchujo, ushindi ambao kila mmoja unamruhusu kuimarisha kambi yake.
Imechapishwa:
Ushindi wa Donald Trump katika jimbo la Florida umepelekea Marco Rubio, Seneta wa Jimbo hilo, kujiondoa mbio za urais kwa tiketi ya chama cha Republican. John Kasich kwa upande wake amejipatia ushindi wake wa kwanza katika jimbo lake la Ohio.
Hawa hapa ni washindi,jimbo kwa jimbo, katika kura za mchujo za Jumanne hii, kulingana na makadirio ya runinga za Marekani:
- Florida
Republican: Donald Trump
Democratic: Hillary Clinton
- Ohio
Republican John Kasich
Democratic: Hillary Clinton
- North Carolina
Republican: Donald Trump
Democratic: Hillary Clinton
- Illinois
Republican: Donald Trump
Democratic: Hillary Clinton
- Missouri
Republican: bado hawajatanza
Democrats: bado hawajatangaza
- IDADI YA USHINDI -
Democrats:
Hillary Clinton: 4
Bernie Sanders: 0
Republican:
Donald Trump: 3
John Kasich: 1
Ted Cruz: 0
Marco Rubio: 0