Pata taarifa kuu
MAREKANI-CUBA-USHIRIKIANO-DIPLOMASIA

Marais wa Marekani na Cuba watazamiwa kukutana

Mkutano wa Amerika, ambao unaanza Ijumaa wiki hii hii katika mji wa Panama, unaweza kuwa kama ulivyoelezwa wa kihistoria kwa sababu ni mara ya kwanza Cuba kushiriki mkutano huo.

Mawaziri wa mambo ya nje wa Marekani na Cuba, John Kerry (kulia) na Bruno Rodriguez (kushoto), wakati wa mazungumzo ya kihistoria katika mji wa Panama, mwezi Aprili 2015.
Mawaziri wa mambo ya nje wa Marekani na Cuba, John Kerry (kulia) na Bruno Rodriguez (kushoto), wakati wa mazungumzo ya kihistoria katika mji wa Panama, mwezi Aprili 2015. REUTERS/U.S. State Department/Handout
Matangazo ya kibiashara

Inaarifiwa kuwa marais wa Marekani na Cuba wanatazamiwa kutana katika mkutano huo. Uhusiano kati ya Marekani na Cuba ulikua ulikatizwa kwa kipindi cha nusu karne, baada ya Marekani kuiwekeza Cuba vikwazo ikiituhumu kufadhili Ugaidi.

Siku chache baada ya rais wa Marekani Barack Obama kuthibitisha kufunguliwa kwa ubalozi wa nchi yake nchini Cuba kuanzia mwezi Aprili huu wa Aprili, hatimaye anatazamiwa kukutana kwa mazungumzo ya ana kwa ana na kiongozi wa nchi hiyo nchini Panama ijumaa wiki hii.

Mwanadiplomasia wa cheo cha juu wa Marekani katika nchi za Marekani ya kusini Roberta Jacobson, alisema kuwa itawezekana kufunguliwa kwa ubalozi kabla ya mkutano wa kimaeneo unaofanyika leo Ijumaa.

Mkuu wa ujumbe wa Cuba Josefina Vidal amesisitiza kuwa Marekani ni lazima iondoe Cuba kutoka kwa orodha ya nchi ambazo zinaunga mkono Ugaidi kabla ya kurejesha tena uhusiano huo.

Mwezi Disemba Cuba na Marekani walitangaza kuwa walikubaliana kuboresha uhusiano wao baada ya zaidi ya miaka 50.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.