Pata taarifa kuu
CHINA-WHO-CORONA-AFYA

WHO yautaja ugonjwa wa Corona kama 'adui wa kwanza kwa umma'

Shirika la Afya Duniani WHO limetangaza kwamba ugonjwa unaofahamika kama Corona, ambao hatimaye unaitwa "Covid-19" ni "tishio kubwa kwa ulimwengu mzima" na unapaswa kuchukuliwa na jamii ya kimataifa kama "adui wa kwanza kwa umma".

mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani, Tedros Adhanom Ghebreyesus ametoa wito wa kugawana sampuli za virusi na kuongeza kasi kwa kutafuta matibabu na chanjo.
mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani, Tedros Adhanom Ghebreyesus ametoa wito wa kugawana sampuli za virusi na kuongeza kasi kwa kutafuta matibabu na chanjo. Fabrice COFFRINI / AFP
Matangazo ya kibiashara

Akiongea kwenye semina iliyohudhuriwa na watafiti zaidi ya 400 na wawakilishi wa mamlaka za afya za kitaifa huko Geneva, mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani, Tedros Adhanom Ghebreyesus ametoa wito wa kugawana sampuli za virusi na kuongeza kasi kwa kutafuta matibabu na chanjo.

"Wakati 99% ya visa vya virusi hivyo vinatokea nchini China, bado hali hii inasalia kuwa janga la dharura kwa nchi hiyo, lakini pia na kutoa kitisho kikubwa kwingineko duniani", Tedros Adhanom Ghebreyesus amebainisha.

Virusi hivyo vilivyotambulika kwa mara ya kwanza katika mji wa Wuhan Desemba 31, vimeuwa zaidi ya watu 1,000, na zaidi ya watu 42,000 wameambukiwza virusi vya ugonjwa huo na kusambaa katika nchi 25.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.