Pata taarifa kuu
ZAMBIA-KIPINDUPINDU-AFYA

Serikali ya Zambia yadhibiti maradhi ya kipindupindu

Shule, makanisa na masoko yamefunguliwa tena baada ya kufungwa kwa muda wa wiki tatu, kutokana na janga la kipindupindu nchini Zambia.

Hospitali kuu ya Lusaka, Zambia, ambako wagonjwa wengi wanaendelea kuhudumiwa.
Hospitali kuu ya Lusaka, Zambia, ambako wagonjwa wengi wanaendelea kuhudumiwa. DAWOOD SALIM / AFP
Matangazo ya kibiashara

Serikali ilikuwa imezuia mikutano ya watu, kwa hofu ya kusambaa kwa ugonjwa huo hatari.

Kipindupindu kimesababisha vifo vya zaidi ya watu 70 nchini humo tangu mwezi Septemba mwaka uliopita.

Mwishoni mwa wezi Desemba 2017, Rais Edgar Lungu wa Zambia, aliamuru vikosi vya kijeshi na polisi wasaidiane na maafisa wa matibabu katika kukabiliana na mlipuko wa kipindupindu ambacho tayari kilisababisha vifo vya watu zaidio ya 41 katika kipindi cha miezi miwili iliyopita.

Mwanzoni mwa mwezi Januari Wizara ya Afya ya Zambia ilitangaza kuwa, maambuzi ya kipindipindu yameshika kasi kubwa zaidi katika mji mkuu wa nchi hiyo Lusaka.

Taarifa iliyotolewa na maafisa wa serikali ya Zambia ilisema idadi ya watu walioambukizwa maradhi ya kipindupindu ilifika elfu mbili katika mji mkuu wa nchi hiyo Lusaka pekee.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.