Pata taarifa kuu
MAREKANI-MAZINGIRA

Wakaazi wa maeneo yalio karibu na Ziwa Oroville watakiwa kuhama

Watu zaidi ya 130,000 wanaoishi kaskazini mwa jimbo la California katika maeneo ambayo yaliyo karibu na bwawa refu zaidi nchini Marekani linalokabiliwa na hatari ya kubomaka wametakiwa kuhama mara moja.

Maafisa wa Zama Moto wakiangalia moto hatari Blue Cut karibu na eneo la Cajon, kaskazini mwa mji wa San Bernadino, California, Agosti 16, 2016.
Maafisa wa Zama Moto wakiangalia moto hatari Blue Cut karibu na eneo la Cajon, kaskazini mwa mji wa San Bernadino, California, Agosti 16, 2016. RINGO CHIU / AFP
Matangazo ya kibiashara

Mtaro wa uliodhoofishwa na mvua kubwa zilizonyesha katika maeneo hayo huwa ukipitisha maji wakati wa dharura katika bwawa la Oroville. Maafisa wamesema wana hofu ya mtaro huo.

Ni mara ya kwanza kwa Ziwa Oroville kukumbwa na dharura ya aina hiyo katika miaka 50 tangu kujengwa kwa bwawa hilo.

Viwango vya maji katika bwawa hilo vimepanda zaidi kutokana na mvua kubwa pamoja na theluji, baada ya miaka mingi ya kiangazi mjini California.

Wataalam wamegundua kwamba baadhi ya vipande vikubwa vya saruji vilikuwa vimebambuka kutoka kwenye mtaro wa kuondosha maji kwenye bwawa hilo la Orovile.

Itafahamika kwamba hivi karibuni California ilikumbwa na majinga asili hasa majanga ya moto ambao uliteketeza baadhi ya kisitu na manyumba kadhaa na kusababisha maelfu ya watu kuyahama makaazi yao.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.