Pata taarifa kuu
UINGEREZA-TABIA NCHI

Uingereza yaunga mkono mkataba kuhusu mabadiliko ya tabia nch

Uingereza imeridhia mkataba wa Paris juu ya mabadiliko ya tabia nchi na hivyo kujiunga na nchi nyingine zaidi ya 100 katika hatua ambayo wanaharakati wanasema wana matumaini kuwa Rais mteule wa Marekani Donald Trump ataheshimu mpango huo.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco, anaongoza mkutano kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, COP22 (kushoto), na Waziri wa Mazingira wa Ufaransa Ségolène Royal wakati wa ufunguzi wa Mkutano kuhusu mabadiliko ya tabia nchi tarehe 7 Novemba 2016 mjini Marrakech.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco, anaongoza mkutano kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, COP22 (kushoto), na Waziri wa Mazingira wa Ufaransa Ségolène Royal wakati wa ufunguzi wa Mkutano kuhusu mabadiliko ya tabia nchi tarehe 7 Novemba 2016 mjini Marrakech. REUTERS/Youssef Boudlal
Matangazo ya kibiashara

Wajumbe wanaohudhuria mkutano mkubwa wa kimataifa juu ya mabadiliko ya hali ya hewa wanaokutana tangu Jumatano wiki hii mjini Marrakech, nchini Morocco, wametoa wito kwa viongozi wa ngazi za juu wa kisiasa kuonesha dhamira ya dhati katika kupambana na suala hilo.

Wajumbe hao wanakutana huku kukiwa na wasiwasi mkubwa kwamba rais mteule wa Marekani, Donald Trump, anaweza kujaribu kurudisha nyuma ahadi na jukumu la nchi yake ya kukataa gesi chafu.

Mkutano huo unatazamiwa kuhitimishwa eoIjumaa mjini Marrakech, nchini Morocco huku kukiwa na maazimio kadhaa kuhusu mabadiliko ya tabia nchi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.