Pata taarifa kuu
SUDANI-SIASA-USALAMA

Milio ya risasi yasikika katika kambi mbili za idara za usalama Khartoum

Miezi mitano baada ya serikali ya raia nchini Sudani kuundwa, milio ya risasi imesikika katika kambi mbili za idara za usalama jijini Khartoum. Hali ambayo imezua wasiwasi mkubwa miongoni mwa wakaazi wa mji huo. tukio lililotokea Jumatatu mchana Januari 14.

Makao makuu ya idara ya ujasusi ya Sudani, Januari 14, 2020 huko Khartoum.
Makao makuu ya idara ya ujasusi ya Sudani, Januari 14, 2020 huko Khartoum. © ASHRAF SHAZLY / AFP
Matangazo ya kibiashara

Kwa mujibu wa ikulu ya rais, hali hiyo imetokea katika moja ya kitengo cha idara ya ujasusi, ambacho kinatarajiwa kuvunjwa, ambapo baadhi ya maafisa wa usalama wenye hasira walijaribu kuandamana.

Tukio hilo lilizua wasiwasi mkubwa katika mji wa Khartoum. Milio mingi ya ya risasi ilisikika Januari 14, huku barabara zikifungwa, wanajeshi wengi walitumwa katika maeneo mbalimbali ya mji na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Khartoum ulifungwa kwa muda wa saa chache.

Ikulu ya rais imebaini kwamba hali hiyo imezushwa na askari waliokataa kulipwa fidia waliyopewa wakati wa kustaafu kwao na kwamba mazungumzo yanaendelea.

Inaonekana makabiliano yalitokea kati ya vikosi vya serikali, jeshi au Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) na idaya ya ujasusi (NISS). Mkuu wa kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) anamtuhumu Salah Gosh, mkuu wa zamani wa idara ya ujasusi (NISS) na moja wa vigogo katika utawala wa Omar al-Bashir, kuwa anahusika katika mstari wa mbele na hali hiyo.

Kwenye ukurasa wake wa Twitter, Waziri Mkuu Abdalla Hamdok amewahakikishia raia kwamba kila kitu kiko chini ya udhibiti na kwamba vikosi vya jeshi vya Sudan vina uwezo wa kushughulikia hali hiyo.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.