Mkuu wa Majeshi aliyeshinikiza kujiuzulu kwa Bouteflika afariki dunia
Mkuu wa majeshi nchini Algeria Ahmed Gaid Salah, ambaye alipata umaarufu mkubwa baada ya kumwambia rais wa zamani Abdelaziz Bouteflika ajiuzulu, amefariki dunia.
Imechapishwa:
Jenerali Salah, mmoja wa wapiganaji wa zamani wa nchi hiyo wakati wa vita vya uhuru kati ya mwaka 1954 hadi 1962, dhidi ya Wafaransa, amefariki dunia baada ya kupata mshtuko wa moyo.
Baada ya kujiuzulu kwa Bouteflika mwezi Aprili, Jenerali Salah alichukua madaraka kwa muda katika kipindi cha mpito.
Serikali ya Algeria imetangaza siku tatu za maombolezo na tayari Jenerali Said Chengriha ametangazwa kuwa mkuu mpya wa Majeshi.
Pamoja na kukumbukwa kumshinikiza rais wa zamani Bouteflika kuachia madaraka, alishirilki pakubwa kuandaa Uchahizi wa urais uliofanyika mwezi huu, licha ya maandamano makubwa ya kupinga uchaguzi huo.