Askari wa tatu na magaidi watatu wauawa kaskazini mwa Burkina Faso
Wanajeshi watatu wa Burkina Faso wameuawa Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo, wakati huu ripoti za kijeshi zikisema kuwa, magaidi 20 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa.
Imechapishwa:
Jeshi linasema, usiku wa kuamkia tarehe mbili na tatu, katika maeneo ya Toeni na Bahn, Kaskazini mwa Burkina Faso, kulitokea shambulizi lililotekelezwa na magaidi.
Katika makabiliano hayo, wanajeshi wengine saba walijeruhiwa na silaha za magaidi hao kama bastola na pikipiki zilikamatwa.
Jumapili, iliyopita, Wakirirsto 14 waliuawa baada ya kushambuliwa wakiwa katika ibada Kanisani, katika mpaka wa nchi hiyo na Nigeria.
Licha ya Burkina Faso kuwa na wanajeshi kutoka Ufaransa, pamoja na wengine kutoka nchi za Sahel kama Mali, Burkina Faso, Niger, Mauritania, Chad na wale wa Umoja wa Mataifa (MINUSMA), hali ya usalama bado ni mbaya.