Chimbuko la kundi la waasi wa ADF mashariki mwa DRC
Imechapishwa:
Cheza - 20:53
Changu chako chako changu, juma hili imeangazia chimbuko la kundi la waasi wa kiislamu wa Uganda, Allied Democratic Forces (ADF) lenye chimbuko lake nchini Uganda lakini kwa sasa limejichimbia mashariki mwa DRCongoWaasi hao wanadaiwa kutekeleza mauaji ya mara kwa mara ya raia mashariki mwa nchi hiyo, miaka kadhaa baada ya kundi hilo kuanzisha uasi kwa lengo la kuung’oa utawala wa rais Yoweri Museveni mnamo miaka ya 1990 lakini ulifurushwa na kuingia DRC.ADF imeendesha vita vya kikatili dhidi ya wakaazi wa Kongo Mashariki na linatajwa kuwa kundi la kigaidi na Umoja wa Mataifa.Kupata mengi zaidi, unagana na mwandishi wetu Reuben Lukumbuka