Pata taarifa kuu
TANZANIA-MSUMBIJI-USALAMA

Tanzania yaandelea kuwasaka watu waliohusika na shambulizi lililoua watu sita

Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya usalama nchini Tanzania, vinaendelea kufanya uchunguzi ili wahusika wa shambulizi lililosababisha mauaji ya watu sita wanakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Moja ya vitongoji Tanzania, ambapo wengi wanasema wahalifu wamekuwa wakiingia nchini Tanzania na kutekeleza uhalifu, baada ya kuishi kwa muda wa kutosha katika baadhi ya maeneo nchini humo..
Moja ya vitongoji Tanzania, ambapo wengi wanasema wahalifu wamekuwa wakiingia nchini Tanzania na kutekeleza uhalifu, baada ya kuishi kwa muda wa kutosha katika baadhi ya maeneo nchini humo.. Getty Images/Peter Adams
Matangazo ya kibiashara

Watanzania sita waliuawa kwa kupigwa risasi na wengine saba kujeruhiwa katika shambulio lililofanywa na washambuliaji wasiojulikana katika kijiji kinachopakana na mkoa mmoja nchini Msumbiji unaojulikana kwa shughuli za kijihadi.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa makosa ya jinai nichi Tanzania, Robert Boaz, amesema wanaliofanya shambulizi hilo walikimbilia msumbiji na bado wanawatafuta

Kwa karibu miaka miwili, wanajihadi wamefanya mshambulizi kadhaa katika mkoa wa Cabo Delgado nchini Msumbiji, unaopakana na Tanzania, na kuwauwa raia wasiopungua 300 na kusabaisha makumi kwa maelfu ya watu kukimbia makazi yao nchini Msumbiji.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.