Pata taarifa kuu
MUGABE-ZIMBABWE-SIASA-HISTORIA

Historia ya maisha na siasa za Robert Mugabe

Robert Mugabe alizaliwa mwezi Februari mwaka 1924, katika familia ya Kikristo ya Katoliki katika eneo la Kutama, Kaskazini Magharibi mwa jiji kuu Harare, wakati huo Zimbabwe ikifahamika kama Southern Rhodesia.

Marehemu  Robert Mugabe rais wa zamani wa Zimbabwe
Marehemu Robert Mugabe rais wa zamani wa Zimbabwe REUTERS/Denis Balibouse/File Photo TPX IMAGES OF THE DAY
Matangazo ya kibiashara

Waliomfahamu vema akiwa mtoto, wanasema alipenda sana kusoma vitabu hata wakati alipokuwa anachunga mifugo msituni.

Miaka ya sitini, alianza harakati za kupigania nchi yake kuwa huru kutoka mikononi kwa Wazungu wachache kutoka nchini Uingereza waliokuwa wanatawala taifa lenye idadi kubwa ya Waafrika.

Harakati zake za kutaka waafrika kujiongoza na kumiliki ardhi, zilisababisha akafungwa jela miaka 10 na serikali ya wakoloni kati ya mwaka 1964 hadi 1974.

Baada ya kuachiliwa huru, alikimbilia nchini Msumbiji na kuunda vuguvugu la ZANU PF kuanizisha vita vya msituni kupambana na serikali ya kikoloni, wakati huo ikiongozwa na Waziri Mkuu Ian Smith.

Wakati huo wa mapambano ya msituni, serikali ya Uingereza ilianzisha mchakato wa mazungumzo na vuguvugu hilo, na kupelekea usitishwaji wa mapigano na Uchaguzi ukafanyika mwaka 1980.

ZANU PF kilishinda Uchaguzi huo na Mugabe kuwa Waziri Mkuu wa kwanza mweusi nchini Southern Rhodesia ambayo ilibadilishwa njia na kuitwa Zimbabwe.

Baadaye, wadhifa wa Waziri Mkuu uliondolewa na Mugabe akawa rais wa nchi hiyo kwa zaidi ya miaka 30 hadi alipolazimishwa kuondoka madarakani na jeshi mwezi Novemba mwaka 2017.

Wengi watamkumbuka Mugabe kama mpiganiaji huru wa Zimbabwe na kiongozi ambaye alipigania umoja wa bara la Afrika na kuwasaidia wananchi wa taifa lake kupata mashamba na elimu.

Hata hivyo, kuna wale watakaomkumbuka kama dikteta, aliyekiuka haki za binadamu na kuminya demokrasia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.