Pata taarifa kuu
SUDANI-SIASA-USALAMA

Mkataba kuhusu taasisi za mpito kutiliwa saini Agosti 17 Sudan

Wananchi wa Sudan wamekuwa wakisherehekea hatua iliyofikiwa kati ya utawala wa kijeshi na viongozi wa maandamanoJumapili wiki hii kuelekea utiwaji saini rasmi tarehe 17 mwezi huu, siku ambayo rais wa zamani Omar Al Bashir anatarajiwa kupelekwa Mahakamani.

Wananchi wa Sudan washerehekea hatua ya utiliaji saini kati ya uatawala wa kijeshi na viongozi wa maandamano.
Wananchi wa Sudan washerehekea hatua ya utiliaji saini kati ya uatawala wa kijeshi na viongozi wa maandamano. Ebrahim HAMID / AFP
Matangazo ya kibiashara

Inatarajiwa kuwa baada ya tarehe 17 wanajeshi na viongozi wa serikali wataunda serikali hiyo ya mpito.

Wanajeshi na viongozi wa waandamanaji nchini Sudan, hatimaye wametiliana saini mkataba wa kikatiba utakaowaongoza katika serikali ya mpito, baada ya miezi saba ya mzozo wa kisiasa.

Mkataba huo unaweka wazi namna taifa hilo litakavyoelekea katika serikali ya kiraia, baada ya serikali ya mpito kumalizika baada ya miaka mitatu.

Kiongozi wa waandamanaji Ahmed Rabie na naibu kiongozi wa Baraza la Kijeshi Jenerali Mohamed Hamdan Daglo, ndio waliotia saini mkataba huo ulioshuhudiwa na wasuluhishi kutoka nchini Ethiopia na Umoja wa Afrika.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.