Pata taarifa kuu
DRC-SIASA-CENI-UCHAGUZI

Naibu mwenyekiti wa CENI nchini DRC ajiuzulu

Naibu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo CENI, Norbert Basengezi ametangaza kujiuzulu wadhifa wake.

Makao makuu ya Tume ya Uchaguzi nchini DRC, CENI
Makao makuu ya Tume ya Uchaguzi nchini DRC, CENI REUTERS/Baz Ratner
Matangazo ya kibiashara

Basengezi amechukua hatua hiyo wakati huu anapoendelea kukabiliwa na vikwazo kutoka kwa Marekani.

Marekani ilichukua hatua hiyo baada ya kuchelewesha matokeo ya Uchaguzi wa urais uliofanyika mwezi Desemba mwaka 2018.

Taarifa kutoka Tume ya Uchaguzi CENI, imesema kuwa Basengezi amewasilisha barua kwa rais Felix Tshisekedi.

Hata hivyo, ni lazima rais Tshisekedi  akubali kujiuzulu kwake.

Aliyekuwa mgombea wa upinzani Martin Fayulu ameendelea kuishtumu Tume ya Uchaguzi kwa kumuibia kura na kumpa ushindi Tshisekedi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.