Waasi zaidi ya sita wauawa katika mapigano na vikosi vya jeshi DRC
Wapiganaji 6 wa waasi wameripotiwa kuuawa mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika makabiliano na wanajeshi wa Serikali (FARDC).
Imechapishwa:
Kwa mujibu wa taarifa kutoka nchini DRC, kundi la waasi waliokuwa na silaha walivamia kijiji kimoja kwenye jimbo la Ituri na kuua watu sita huku kukiwa na hofu kuwa mamia ya raia wametekwa.
Msemaji wa jeshi la DRC amelaani shambulio hilo linalodaiwa kutekelezwa na wapiganaji wa kundi la ADF.
Taarifa zaidi zinasema kuwa wanajeshi wa Serikali walikabiliana na waasi hao kwa zaidi ya saa moja kabla ya kuwashinda nguvu ambapo wameripoti kuwaua wapiganaji zaidi ya 6.
Kiongozi mmoja wa kijadi kwenye eneo hilo amesema mpaka sasa watu 30 hawajulikani walipo na wanahofu kuwa huenda walitekwa nyara na waasi hao huku zaidi ya ngombe 100 pia wakichukuliwa.