Fayulu awataka wafuasi wake kuendelea na vita vya kisiasa kwa amani
Mgombea wa upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Congo Martin Fayulu ametupilia mbali juhudi za rais mpya wa nchi hiyo Felix Tshisekedi ambaye ameonyesha nia ya kutaka maridhiano, akisema "unapopewa mkono ambao ni mchafu, hupaswi kupokea".
Imechapishwa:
Mgombea wa upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Congo Martin Fayulu ametupilia mbali juhudi za rais mpya wa nchi hiyo Felix Tshisekedi ambaye ameonyesha nia ya kutaka maridhiano, akisema unapopewa mkono ambao ni mchafu, huupokei.
Akiwahutubia maelfu ya wafuasi wake kwa mara ya kwanza tangu kushindwa kwenye uchaguzi wa Desemba 30 mwaka jana, Fayulu amewaambia wafuasi wake waliokusanyika mjini Kinshasa mwishoni mwa juma lililopita, kuwa hatatumia fujo anapoendelea kupinga uchaguzi anaodai ulikumbwa na udanganyifu.
Fayulu amesema jaji mmoja wa Mahakama ya Katiba amejitokeza na kuweka wazi kuhusu kilichofanyika,
Katika hatua nyingine Martin Fayulu ameongeza kuwa ameapa kushinikiza Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika kutoheshimu amri kutoka kwa mtu anayedai hahuchaguliwa.