Pata taarifa kuu
DRC-FARDC-USALAMA

Jeshi la DRC laua wanamgambo saba Ituri

Wanamgambo sita na kiongozi wao wameuawa wakati wa operesheni ya kijeshi katika mkoa wa Ituri, Kaskazini Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), jeshi la DRC limesema katika taarifa yake.

Askari wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (FARDC) wakipiga doria katika kijiji cha Kaswara, kilomita 60 kusini magharibi mwa Bunia, katika mkoa wa Ituri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Julai 14, 2006.
Askari wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (FARDC) wakipiga doria katika kijiji cha Kaswara, kilomita 60 kusini magharibi mwa Bunia, katika mkoa wa Ituri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Julai 14, 2006. REUTERS
Matangazo ya kibiashara

" Tumeshambulia ngome ya wanamgambo wa Mai-Mai Simba usiku wa Jumatatu kuamkia Jumanne na tumeuawa wanamgambo saba, ikiwa ni pamoja na kiongozi wao Manu", Luteni Jules Tshikudi, msemaji wa Jeshi la FARDC katika mkoa wa Ituri (kaskazini mashariki) ameliambia shirika la Habari la AFP.

Operesheni hiyo imefanyika katika eneo la Pembele, kilomita10 kutoka Nyanya katika wilaya ya Mambasa, magharibi mwa Bunia.

Taarifa hii ya kuuawa kwa wanamgambo saba imethibitishwa na Mkuu wa wilaya ya Mambasa Mambasa, Idris Lokodila.

"Wakazi wanafurahi kusikia kuwa Manu ameuawa, kiongozi wa waasi aliyetesa wananchi," Bw Lokodila amesem.

Manu, ambaye jina lake halisi halijulikani, alichukua mikoba ya Paul Sadala, kwa jina maarufu Morgan, ambaye aliuawa mnamo mwaka 2014.

anashtumiwa kuendesha ujangili katika hifadhi ya Okapi, eneo la Epulu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.