Watatu wauawa katika maandamano Omdurman, Sudan
Watu watatu wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya polisi kuingilia kati kwa kutawanya maandamano ya kupinga serikali katika mji wa Omdurman, mji ulio karibu na mji mkuu wa Sudan, Khartoum, msemaji wa polisi amesema.
Imechapishwa:
"Mkusanyiko uliopigwa marufuku ulifanyika Omdurman na polisi ilitawanywa waandamanaji kwa mabomu ya machozi," Hashim Abdelrahim msemaji wa polisi amesema katika taarifa hiyo.
"Kabla, polisi walitambua vifo vya waandamanaji watatu na umeanzisha uchunguzi," Bw Abdelrahim amesema bila kutoa maelezo zaidi.
Siku ya Jumatano, chanzo cha hospitali kiliambia shirika la Habari la AFP kwamba mtu mmoja alifariki kutokana na majeraha alioyapata wakati wa maandamano, huku watu sita wakijeruhiwa kwa risasi katika mji wa Omdurman.
Sudan inaendelea kukumbwa na maandamano kufuatia kupanda kwa bei ya mkate na mdororo wa uchumi unaoendelea. Kwa sasa waandamanaji wanaomba rais Omar Al Bashir ajiuzulu.