Uchaguzi DRC: Vituo kadhaa vya kupigia kura vyachomwa moto Inongo
Uchaguzi Mkuu nchini DRC ambao umefanyika katika maeneo mbalimbali nchini humo umeingiliwa na dosari, huku mashrika mbalimbali yakikosoa namna uchaguzi huo ulivyoandaliwa.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Baadhi ya vituo vya kupigia kura vimefungwa huku, vingine vikichomnwa moto kwa tuhuma za udanganyifu.
Kwa mujibu wa mwandishi wetu wa habari Sonia Rolley, katika eneo la Inongo, vituo viwili vya kupigia kura ndivyo vimefanya kazi, vingine vimechomwa moto baada ya tuhuma za udanganyifu.
#RDC #Elections : à Inongo, il n’y a plus que deux centres de vote fonctionnent, tous les autres ont été détruits après des soupçons de fraude. « Une machine qu’on présentait comme une machine de réserve était utilisée par la Presidente d’une bureau pour tricher »
Sonia Rolley (@soniarolley) December 30, 2018
Wakati huo huo Baraza Kuu la Maaskofu wa kanisa Katoliki nchini DRC (Cenco), katika taarifa yake, limebaini kwamba jumla ya vituo vya kupigia kura 12 300 walivyoorodhesha (56%): vituo vya kupigia kura 846 vimewekwa katika maeneo yaliyokatazwa. Ripoti 1,543 za matukio mabaya ikiwa ni pamoja na kesi 544 za matatizo ya mashine za kupigia kura, kesi 115 za wawakilishi mbalimbali kukataliwa kuingia katika vituo vya kupigia kura, kesi 86 za kufukuzwa kwa mashahidi, kesi 44 za rushwa, kesi 194 za vifaa kuharibiwa.
#RDC #Elections : sur 12300 reçus (56%) : 846 bureaux de vote dans des lieux prohibés. 1543 rapports d’incidents dont 544 pour dysfonctionnement des machines, 115 sur problème accès témoins, 86 pour expulsion de témoins, 44 corruption, 194 vandalisme d’installation pic.twitter.com/fTgL4RH5kQ
Sonia Rolley (@soniarolley) December 30, 2018
Mapema mchana wakaazi wa Beni moja ya maeneo ambayo uchaguzi umeahirishwa hadi mwezi Machi mwaka 2019 wamepiga kura hewa ili kupinga uamuzi wa Tume ya Uchaguzi nchini DRC (CENI) kuahirisha uchaguzi katika maeneo matatu ya nchi hiyo Beni, Butembo na Yumbi, Magharibi mwa nchi.
Mashirika ya vijana na wakazi wa Beni wametenga vituo kadhaa vya kupiga kura na wakazi wa mji huo waliitikia wito wa mashirika hayo kuja kupiga kura.
Mapema wiki hii, Tume ya Uchaguzi (CENI) katika taarifa yake imesema, sababu ya uchaguzi huo kuahirishwa hadi mwezi Machi mwaka 2019, ni kwa sababu ya changamoto za kiusalama katika maeneo hayo ambayo yameendelea kushuhudia mashambulizi ya makundi ya waasi.
Wapiga kura milioni 40 wamepiga kura kumchagua rais wao mpya atayemrithi rais anayemaliza muda wake Joseph Kabila Kabange.Tume ya Uchaguzi inasema, mshindi atatangazwa tarehe 15 na kuapishwa tarehe 18 mwezi Januari.
Hakuna duru ya pili ya Uchaguzi nchini DRC, anayeshinda atatangazwa na Tume hiyo.