SUDAN-MAANDAMANO-UCHUMI
Maandamano yaendelea Sudan
Wanafunzi wanaosomea Udakttari katika chuo kikuu cha Gadarif, Mashariki mwa Sudan, wameungana na Madaktari wanaogoma, kushinikiza kujiuzulu kwa rais Omar Al Bashir.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Madaktari wanawataka wafanyikazi wa taaluma nyingine, kujitokeza na kuwaunga mkono katika mgomo huu.
Raia wa kawaida nao wanaendelea kujitokeza katika barabara za miiji mbalimbali kumtaka rais Bashir aondoke madarakani lakini pia wanalalamikia kupanda kwa bei ya mkate na mafuta.
Rais Bashir, amewaita wanaoandamana kama wasaliti.