AFRIKA KUSINI-GRACE MUGABE-HAKI
Grace Mugabe atafutwa na vyombo vya sheria vya Afrika Kusini
Afrika Kusini imetoa hati ya kukamatwa kwa Grace Mugabe, mke wa rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe, kwa madai ya kumpiga mlimbwende Gabriella Engel jijini Johannerburg mwaka uliopita.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Polisi wanamtafuta Bi.Mugabe, baada ya Mahakama kuondoa kinga ya kufunguliwa kwake mashtaka.
Gabriella ambaye anadai alijeruhiwa na Bi. Mugabe alikuwa na watoto wa kiume wa Mugabe, Robert na Chatunga, wakati aliposhambuliwa.
Gabriella Engels alimshutumu Grace Mugabe kwa kumpiga katika chumba cha hoteli mjini Johannesburg.
Serikali ya Afrika Kusini ilikosolewa kwa kuruhusu Bibi Mugabe kuondoka nchini humo baada ya mashambulizi.