Pata taarifa kuu
GABON-SIASA-AFYA

Rais wa Gabon aonekana hadharani baada ya kulazwa hospitali kwa miezi kadhaa

Rais wa Gabon Ali Bongo, ameonekana hadharani kwa mara ya kwanza, akiwa nchini Morocco, baada ya kuwasilia nchini humo siku chache zilizopita akitokea nchini Saudi Arabia alikokuwa amelazwa.

Rais Bongo ameonekana kwa mara ya kwanza, akiwa na Mfalme Mohammed VI aliyeenda kumtembelea.
Rais Bongo ameonekana kwa mara ya kwanza, akiwa na Mfalme Mohammed VI aliyeenda kumtembelea. © AFP
Matangazo ya kibiashara

Rais Bongo, anapata mapumziko ya baada ya matibabu kabla ya kurejea jijini Libireville, na ameonekana kwa mara ya kwanza, akiwa na Mfalme wa nchi hiyo Mohammed VI aliyeenda kumtembelea.

Ugonjwa unaosumbua, haujawekwa wazi lakini, inaaminika kuwa alipata kiharusi mwishoni mwa mwezi Oktoba, wakati alipokuwa amekwenda nchini Saudi Arabia kuhudhuria mkutano wa kimataifa.

Mnamo Novemba 11, msemaji wa ikulu Ike Ngouoni aliwaambia waandishi wa habari kuwa  rais Ali Bongo  atakuwa mwenye afya nzuri katika siku za hivi karibuni.

Vyombo vya habari nchini Gabon vilikuwa vikifahamisha kuwa huenda rais Ali Bongo akapelekwa mjini Paris au London.

Ali Bongo ni mtoto wa aliekuwa rais wa zamani wa nchi hiyo Omar Bongo ambae aliongoza taifa hilo tangu mwaka 1967  hadi  alipofariki  Juni  8  mwaka 2009.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.