Ziara yake ya kwanza imemfikisha jijini Brazaville nchini Congo ambako amekutana na viongozi mbalimbali na kuahidi kutekeleza ahadi zake wakati wa muhula wake ambao utaanza mwezi Januari.
Aidha, amesema haitasahau nchi yake ya Rwanda.
"Ni wazi kwamba katika kutekeleza majukumu yangu nchi yangu haitatengwa. Rwanda ni nchi yenye lugha nyingi. Umuhimu wa lugha ya Kifaransa - kwa uhakika - utakuwa kipaumbele, "amesema Louise Mushikiwabo.
Baada ya kuzungumza na waandishi wa habari Louise Mushikiwabo amepands ndege na kuelekea katika mji wa Oyo ambako amekwenda kukutana na rais wa Congo Brazaville Dennis Sassou Nguesso.