Pata taarifa kuu
GAMBIA-UKWELI-HAKI-SIASA-MARIDHIANO

Gambia yazindua Tume ya Ukweli Haki na Maridhiano

Gambia imezindua Tume ya Ukweli Haki na Maridhiano, kuchunguza visa vya ukiukwaji wa haki za binadamu vilivyotokea wakati wa rais wa zamani Yahya Jammeh.

Rais wa Gambia  Adama Barrow
Rais wa Gambia Adama Barrow REUTERS/Benoit Tessier
Matangazo ya kibiashara

Tume hiyo hiyo itakuwa na Makamishena 11 ambao tayari wameapishwa jijini Banjul kuanza kazi hiyo.

Kuanzia mwisho wa mwezi Oktoba, watu mbalimbali walioteswa au kunyanyaswa wanatarajiwa kwenda kutoa ushahidi wao mbele ya Tume hiyo.

Shirika la Kimataifa la kutetea haki za Binadamu la Human Rights Watch limesema raia wa nchi hiyo walioteswa, kubakwa wakiwa jela au kulazimishwa kunywa dawa zilizotengezwa na Jammeh ili kuponya maambukizi ya Ukimwi watajitokeza kutoa shuhuda zao.

Rais Adama Barrow amesema kuwa, Tume hiyo itasaidia sana katika uponyaji wa nchi hiyo.

“ Tusimame pamoja kusema, hatutaruhusu tena watu wachache kututesa kama taifa,' aliandika kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Tume hii kama ilivyokuwa ile ya Afrika Kusini, itasikiliza shuhuda dhidi ya watu mbalimbali kipindi chote cha miaka 22 alichoongoza Jammeh ambaye amepewa hifadhi nchini Equitorial Guinea.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.