Pata taarifa kuu
DRC-MAREKANI-HRW-CENCO-UCHAGUZI

Marekani yakosoa kauli za viongozi wa DRC

Hatua za mwisho za mchakato wa uchaguzi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo zimezua wasiwasi kwa Marekani, Kanisa Katoliki na shirika la kimataifa la Haki za Binadamu la Human Right Wacht (HRW).

Nikki Haley wakati wa ziara yake Kinshasa akioongea na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (Ceni), Corneille Nangaa, DRC, Oktoba 27, 2017.
Nikki Haley wakati wa ziara yake Kinshasa akioongea na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (Ceni), Corneille Nangaa, DRC, Oktoba 27, 2017. REUTERS/Robert Carrubba
Matangazo ya kibiashara

"Tuna wasiwasi sana na uamuzi wa Tume ya Uchaguzi wa tarehe 24 Agosti kuwaondoa wagombea wengine wa upinzani katika uchaguzi wa urais kwa kile kinachoonekana kuwa ni sababu za kisiasa," Balozi wa Marekani kwenye Umoja wa Mataifa Nikki Haley alisema mapem awiki hii.

Faili za wagombea urais sita kati ya 25, ikiwa ni pamoja na kiongozi wa zamani wa kivita Jean-Pierre Bemba, hazikupokelewa na Tume ya Uchaguzi (CENI). Sita hao wamewasilisha malalamiko yao kwa Mahakama ya Katiba.

Balozi wa Marekani kwenye Umoja wa Mataifa pia ameitaja kuwa ni "kero" kauli ya rais Joseph Kabila na Tume ya Uchaguzi (CENI) kukataa msaada wowote kutoka nje kwa ajili ya uchaguzi uliopangwa kufanyika Desemba 23.

"Tunaheshimu DRC kama nchi mwanachama wa Umoja wa Mataifa, lakini hiyo inaweza kuchochea uhasama wakati serikali ya DRC inakataa misaada ambayo itasaidia kuandaa uchaguzi huru, wa haki na wa kuaminika," alisema Haley.

Alikua akizungumza katika mkutano wa kufuatilia mchakato wa uchaguzi mbele ya wanachama kadhaa wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, ikiwa ni pamoja na Ufaransa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.