Pata taarifa kuu
AFRIKA KUSINI-ZUMA-HAKI

Afrika Kusini: Kesi ya Zuma yaahirishwa hadi Novemba 30

Mahakama ya Afrika Kusini imeahirisha kwa mara nyingine kesi ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo Jacob Zuma hadi Novemba 30. Jacob Zuma anashtumiwa kashfa ya rushwa katika mkataba wa silaha. Kesi hiyo imeahirishwa ili kuwezesha wanasheria wake wapya kufahamu yaliomo katika kesi inayomkabili mteja wao, kwa mujibu wa chanzo cha mahakama.

Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma katika Mahakama ya Pietermaritzburg, Julai 27, 2018.
Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma katika Mahakama ya Pietermaritzburg, Julai 27, 2018. © AFP
Matangazo ya kibiashara

"Kesi yako imeahirishwa hadi Novemba 30, 2018," Jaji Mjabuliseni Madondo alimwambia mtuhumiwa, ambaye alikua amesimama kizimbani katika mahakama ya Pietermaritzburg, kaskazini mwa Afrika Kusini.

Zuma, mwenye umri wa miaka 76, anashutumiwa kuwa alipokea rushwa kutoka kwa kampuni ya elektroniki na ulinzi Thales katika mkataba wa silaha wenye thamani ya karibu euro bilioni 4 uliyotolewa mwaka 1999.

Jacob Zuma, wakati huo "waziri" wa serikali ya mkoa kisha makamu wa rais wa Afrika Kusini, amekanusha shutma hizo dhidi yake.

Kampuni ya Ufaransa Thales pia imehusishwa katika kesi hiyo.

Mwanasheria wa "Kihistoria" wa Jacob Zuma, Michael Hulley, hivi karibuni alijiondoa kwenye kesi hiyo kwa sababu ya utata kuhusu malipo ya ada yanayohusiana na utaratibu wa mahakama kwa mteja wake ambayo yalitakiwa kulipwa na serikali. Swala ambalo linapaswa kutatuliwa hivi karibuni na mahkama.

Mwanasheria wake mpya amesema leo Ijumaa mbele ya mahakama kwamba anatarajia kuwasilisha ombi la kufuta mashtaka dhidi ya Jacob Zuma lakini ametaka kupewa muda wa mwisho wa kujua undani wa mashitaka yanayomkabili.

"Tutashughulikia kesi hiyo, tupe fursa ya kuweka mambo sawa kwa kesi hii," amesema Michael Hellens.

"Kipindi cha miezi mitatu kitatosha, ikimaanisha kwamba upande wa utetezi utaruhusiwa kuwasilisha maombi yake ifikapo Novemba 16, 2018," Jaji Madondo amesema.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.