Pata taarifa kuu
ZIMBABWE-SIASA-USALAMA

Rais wa Zimbabwe awashtumu wafuasi wa Grace Mugabe kuhusika na shambulizi

Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa amehusisha kundi la wafuasi wa chama tawala cha Zanu PF waliojitenga na ambao wanamuunga mkono mkewe Robert Mugabe na mlipuko wa Jumamosi, mwishoni mwa juma lililopita.

Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa lwakati wa mkutano wa kampeni za uchaguzi za Zanu-PF,  Bulawayo, Juni 23, 2018.
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa lwakati wa mkutano wa kampeni za uchaguzi za Zanu-PF, Bulawayo, Juni 23, 2018. ZINYANGE AUNTONY / AFP
Matangazo ya kibiashara

Mlipuko huo, uliotokea wakati Emmerson Mnangagwa alipokua akiondoka kwenye uwanja alipokua akiendesha mkutano wa kampeni za uchaguzi baada ya kuwahutubia wafuasi wake, ulisababisha vifo vya watu wawili.

Rais, ambaye amemrithi mtangulizi wake Robert Mugabe mnamo mwezi Novemba baada ya kumtenga, amesema anashuku G40, kundi la wafuasi wa Zanu-PF wanaomuunga mkono Grace Mugabe, kwa mujibu wa BBC.

Hajamshtumu Grace Mugabe kushiriki katika shambulizi hilo na amesema anasubiri watu zaidi kukamatwa kufuatia shambulizi hilo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.