Wabunge DRC kutunga sheria ya kuwalinda marais waliostaafu
Wabunge nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, wanatarajiwa kukutana kwa lengo la kutunga sheria ya kuwalinda marais wanaostaafu.
Imechapishwa:
Spika wa bunge Aubin Minaku amesema, rais Kabila ameomba kuwa wabunge wakutane na kujadili na kupitisha sheria hiyo, haraka iwezekanavyo.
Hii ni dalili kuwa huenda rais Kabila ataheshimu Katiba na kutowania tena urais wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwezi Desema, licha ya wasiwasi kuwa huenda akaamua kwuania tena.
Wiki hii, Waziri Mkuu Bruno Tshibala alisema rais Kabila ataheshimu Katiba na hatawania urais kwa muhula wa tatu kinyume na Katiba.
Rais Kabila amekuwa akiongoza nchi hiyo tangu mwaka 2001.