Pata taarifa kuu
DRC-USALAMA-HAKI

Visa vya utekaji nyara kwa watoto vyakithiri Kivu Kusini

Kuanzia mwezi Januari 2017 hadi mwezi Mei 2018, karibu watoto 85 walitekwa nyara katika mkoa wa Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. viongozi tawala katika mkoa huo wamethibitisha hali hiyo.

Mji wa Bukavu Mashariki mwa DRC.
Mji wa Bukavu Mashariki mwa DRC. www.rfi.fr
Matangazo ya kibiashara

Mashirika ya haki za binadamu yameiomba serikali kukomesha hali hii, ambayo inachingia kwa mdororo wa usalama nchini.

Kiongozi wa shirika la haki za binadmu la ASADHO, Joshua Blaise Mukubwa, anasema hali hii inatisha, huku akiwalamu viongozi wa mkoa wa Kivu Kusini kushindwa kudhibiti hali hii.

Kwa mujibu wa Bw Mukubwa maeneo ya pwani ya mkoa wa Kivu Kusini, karibu na Ziwa Kivu na Ziwa Tanganyika, ni maeneo yaalioathirika zaidi na visa hivi vya utekaji nyara kwa watoto ambavyo vilianza kuongezeka tangu mwanzoni mwa mwaka 2018.

Wakati huo huo Idara ya uhamiaji nchini DRC imechukua hatua kwa mtu yeyote anayetaka kuvuka mpaka na mtoto mdogo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.