Pata taarifa kuu
MALI-UCHAGUZI-SIASA

Rais wa Mali atangaza rasmi kuwania katika uchaguzi ujao

Rais wa Mali ametangaza rasmi kwamba atagombea tena urais kwa muhula wa tatu katika uchaguzi mkuu ambao umepangwa kufanyika tarehe 29 mwezi julai mwaka huu, na hivyo kujiunga na wagombea wengine ishirini kwenye nafasi hiyo.

Ibrahim Boubacar Keita, hapa ilikua Mei 10, 2018, ni mgombea rasmi wa urais kwa muhula wa tatu wa miaka mitano.
Ibrahim Boubacar Keita, hapa ilikua Mei 10, 2018, ni mgombea rasmi wa urais kwa muhula wa tatu wa miaka mitano. Sia KAMBOU / AFP
Matangazo ya kibiashara

Rais Ibrahim Boubacar Keita ametoa tangazo hilo kwenye televisheni ta taifa, akisema kuwa amechukua uamuzi huo kutokana na kile anachosema kuwa amefanikiwa kuimarisha uchumi wa taifa.

"Ninatangaza kwamba nitagombea tena urais kwa muhula wa tatu katika uchaguzi mkuu ambao umepangwa kufanyika tarehe 29 mwezi julai mwaka huu."

Rais Keita ameelezea kwa nini ameamua kugombea tena urais kwa muhua wa tatu wa miaka mitano: "Ninaamua kuendelea na kazi yangu ya kutumikia vizuri Mali, wakati huu ambapo hofu na mashaka kwa wananchi bado vinatawala kutokana na kudorora kwa usalama. "

Rais Keita amesifu kazi kubwa aliofanya hasa vita dhidi ya ugaidi, huku akibaini kwamba amiimarisha jeshi lake na kulipa uwezo wa kutosha katka kulinda usalama a raia, huku akisifu pia kwa njia moja ama nyingine alivyochangia kwa kiasi kikubwa ili kufikia makubaliano ya amani na maridhiano kutokana na mchakato wa Algiers. "

Katika hotuba yake ya dakika 14, Ibrahim Boubacar Keïta amesema kuwa alisikia malalamiko kutoka kwa wananchi wa Mali ambao walidai kutoridhishwa na baadhi ya mambo katika utawala wangu, hasa utawala bora.

"Jitihada zimefanywa, hata hivyo, lakini hazijazaa matunda yanayohitajika. "

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.