Pata taarifa kuu
ZIMBABWE-SIASA-HAKI

Zimbabwe yajiandalia uchaguzi

Mahakama maalum zimeundwa nchini Zimbabwe ili kusikiliza na kuhumu kesi kuhusu machafuko yatakayotokea baada ya kipindi cha Uchaguzi.

Baada ya miezi kadhaa Emmerson Mnangagwa kuchukua hatamu ya uongozi wa nchi, Mahakama maalum zimeundwa nchini Zimbabwe ili kusikiliza na kuhumu kesi kuhusu machafuko yatakayotokea baada ya kipindi cha Uchaguzi.
Baada ya miezi kadhaa Emmerson Mnangagwa kuchukua hatamu ya uongozi wa nchi, Mahakama maalum zimeundwa nchini Zimbabwe ili kusikiliza na kuhumu kesi kuhusu machafuko yatakayotokea baada ya kipindi cha Uchaguzi. REUTERS/Philimon Bulawayo
Matangazo ya kibiashara

Uzinduzi huu umefanyika kuelekea Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika mwezi Julai.

Utakuwa ni Uchaguzi wa kwanza bila ya rais wa zamani wa nchi hiyo Robert Mugabe aliyetimuliwa madarakani mwaka uliopita.

Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa alitangaza kwamba Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika mwaka huu nchini Zimbabwe unapaswa kufanyika "kabla ya mwezi Julai". Tangazo hili alilitoa katika mkutano wa kiuchumi duniani uliofanyika Davos, nchini Uswisi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.