Pata taarifa kuu
ANGOLA-USALAMA

Rais wa Angola amtimua mkuu wa majeshi

Rais wa Angola Joao Lourenco amemfuta kazi Mkuu wa Majeshi Jenerali Geraldo Sachipengo Nunda, baada ya kutajwa katika kashfa ya ufisadi.

Rais wa Angola João Lourenço.
Rais wa Angola João Lourenço. JOOST DE RAEYMAEKER/LUSA
Matangazo ya kibiashara

Kiongozi huyo aliyeingia madarakani mwezi Septemba mwaka uliopita, amekuwa akiachana na waliokuwa washirika wa rais wa zamani Jose Eduardo dos Santos aliyeongoa nchi hiyo kwa miaka 37.

Mnamo mwezi Novemba mwaka jana Lourenco alimfuta kazi kamanda wa jeshi la polisi Ambrosio de Lemos na mkuu wa upelelezi (usalama wa taifa) Antonio Jose Maria katika mabadiliko makubwa ya kwanza ya vyombo vya usalama tangu tangu alipoingia madarakani mwezi Septemba mwaka jana.

Miezi michache baadae alimfuta kazi binti wa rais wa zamani Isabel Dos Santos ambaye alikuwa mkuu wa kampuni ya mafuta nchini humo na mwanamke tajiri zaidi barani Afrika kinyume na matarajio ya wengi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.