Pata taarifa kuu
ICC-DRC

Mahakama ya ICC kuamua rufaa ya Germain Katanga

Majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya ICC mjini Hague nchini Uholanzi, siku ya Alhamisi, wataamua rufaa iliyowasilishwa na Germain Katanga kiongozi wa zamani wa kundi la waasi la FRPI nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Germain Katanga kiongozi wa zamani wa waasi nchini DRC
Germain Katanga kiongozi wa zamani wa waasi nchini DRC www.icc-cpi.int
Matangazo ya kibiashara

Mwaka 2014, Mahakama ya ICC ilimhukumu Katanga miaka 12 jela baada ya kumpata na makosa matano ikiwemo vita vya uhalifu na makosa mengine ya ukiukwaji wa haki za binadamu ikiwemo mauaji na ubakaji.

Katanga alipatikana na kosa la kutekeleza makosa hayo dhidi ya maelfu ya wakaazi wa kijiji cha Bogoro mwaka 2003 katika jimbo la Ituri.

Mwaka 2017, Mahakama ya ICC iliamua kuwa watu 300 walioathiriwa na mashambulizi ya waasi hao, kila mmoja atalipwa dola 250 kama fidia.

Katanga anasema Majaji kubadilisha uamuzi huo wa kulipa fidia waathiriwa hao, kwa sababu hana fedha zozote za kutoa malipo hayo.

Katanga anakitumia kifungo hicho nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.