Pata taarifa kuu
COTE D'IVOIRE-USALAMA

Cote d'Ivoire yasikitishwa na uvamizi dhidi ya kambi ya kijeshi ya Bouake

Kambi moja ya jeshi kwenye mji wa Bouake nchini Cote d'Ivoire ambako mwaka jana kulishuhudiwa uasi wa wanajeshi, imevamiwa na kuharibiwa na wanajeshi wa Serikali.

Wataalam wa kijeshi wa Ufaransa wamekua wakipendekeza kitoa kuepo na mfumo wa kutoa mafunzo ya kijeshi kwa jeshi la Cote d'Ivoire.
Wataalam wa kijeshi wa Ufaransa wamekua wakipendekeza kitoa kuepo na mfumo wa kutoa mafunzo ya kijeshi kwa jeshi la Cote d'Ivoire. © Frédéric Garat
Matangazo ya kibiashara

Milio ya risasi ilisikika Jumanne usiku kwenye kambi hiyo wakati wanajeshi kutoka kambi nyingine walipovamia kambi hiyo yenye wanajeshi wa kikosi maalumu na kuanza kuharibu ofisi na kuchoma moto magari.

Msemaji wa Serikali ya Cote d'Ivoire, Bruno Kornee, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa, hali ya utulivu tayari imerejea kwenye mji huo.

Tukio hili jipya lilijadiliwa katika kikao cha Baraza la Mawaziri cha siku ya Jumatano, Januari 10. Mawaziri wote walielezea masikitiko yao kutokanna na uvamizi huo.

Hivi karibuni rais Allasane Ouattara alitangaza kuanza kutekeleza mabadiliko ya kuwapunguza mamia ya wanajeshi waasi waliomsaidia kuingia madarakani ili kutengeneza jeshi la kitaifa hatua ambayo imezusha hofu ya kutokea uasi mwingine.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.