DRC yakanusha ripoti ya Human Right Watch kuhusu M23
Shirika la kimataifa la haki za binadamu la Human Right Watch limemtuhumu rais Joseph Kabila wa DRC kuwasajili wapiganaji wa zamani wa kundi la M23 kwa lengo la kuwakandamiza waandamanaji waliokuwa wakipinga utawala wake Desemba 19 na 20 mwaka 2016 jijini Kinshasa.
Imechapishwa:
Kwa mujibu wa shirika hilo, ukandamizaji zilisababisha vifo vya watu 60.
Serikali ya DR Congo kupitia waziri wake wa haki za binadamu Marie Ange Mushobeka, amesema ameshangazwa na ripoti hiyo na kwamba shirika hilo halina ushahidi wowote kuhusu tuhuma hizo.
#RDC #Rwanda #Ouganda : sur la méthodologie, pour réaliser ce rapport @hrw, 120 témoignages, dont 13 combattants du #M23 recrutés et 9 officiers et membres des services de securité qui auraient tous confirmé ce recrutement - https://t.co/aoCbWQHRac pic.twitter.com/KCFlJ28uaD
Sonia Rolley (@soniarolley) 4 décembre 2017
Hata hivyo Human Wright Watch inasema ilikusanya ushahidi kupitia watu mbalimbali wakiwemo wapiganaji hao waliotoa ushuhuda kama anavyoeleza hapa Ida Soyere mkurugenzi wa Human Right Watch katika ukanda wa Afrika ya kati.
Upande wake Waziri wa Ulinzi nchini DR Congo, Crispin Atama Thabe, amesema tuhuma hizo zimekuja ili kulichafuwa jeshi na kuharibu uaminifu na kwamba, wakati wa mapigano dhidi ya kundi hilo maafisa kadhaa wa FARDC walipoteza maisha, hivyo hawana sababu ya kuwatumia wanajeshi hao.
Naye kiongozi wa zamani wa kundi la M23 Bertrand Bisimwa amesema serikali ya Congo imewaajiri kupitia mlango wa nyuma wapiganaji wa zamani walioasi kundi hilo waliofukuzwa.
Our response to HRW: The recruitment and the use by the Drc Government of the deserters and other undiscipled expelled by the M23 for the purposes of repressing the citizen’s protest have as sole motivation to keep our organisation away from the people; which is unacceptable. pic.twitter.com/6E8IulIagL
Bertrand Bisimwa (@bbisimwa) 5 décembre 2017