CENI kutangaza kalenda ya uchaguzi mwishoni mwa juma hili
Tume Huru ya Uchaguzi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo-DRC, CENI inatarajiwa kutoa kalenda ya uchaguzi mwishoni mwa juma hili licha ya Tume hiyo hapo awali kutoa angalizo kuwa uchaguzi hauwezi kufanyika kabla ya mwaka 2019.
Imechapishwa:
Hayo yanajiri wakati huu hali ya joto la kisiasa ikiendelea kupanda kwa Rais Joseph Kabila kutakiwa kuondoka madarakani kwa kuheshimu makubaliano ya Desemba 31 mwaka jana huku Marekani ikishinikiza uchaguzi ufanyike 2018.
Hivi karibuni Naibu Mwenyekiti wa CENI, Norbert Basengezi ameripotiwa akisema kuwa ukalenda ya Uchaguzi itatolewa mwishoni mwa juma hili na kwamba makubaliano ya Desemba 31 yataheshimiwa.
Norbert Basengezi amesema kuwa tayari tume yake imekutana na wajumbe wa kamati inayoratibu utekelezwaji wa makubaliano hayo pamoja na wajumbe wa serikali ili kuafikiana kuhusu kalenda ya uchaguzi.