Habari RFI-Ki
Baadhi ya Wabunge wa chama NRM waungana upinzani nchini uganda kupinga uwasilishwaji wa muswada tata
Imechapishwa:
Cheza - 09:40
Wabunge wa chama tawala nchini Uganda NRM, wameshindwa kuwasilisha mswada wa kuibadilisha katiba kuondoa kikomo cha umri kwa yeyote anayetaka kuwa rais nchini humo.Baadhi ya wabunge wa chama tawala wameungana na upinzani kupinga uwasilishwaji wa mswada huu tata.Mvutano mkali hapo jana bungeni ulisababisha vikao vya bunge kuahirishwa hadi Jumanne wiki ijayo. Una maoni gani kuhusu kinachoendelea nchini Uganda?