Pata taarifa kuu
DRC-EBOLA

DRC yasema haina tena maambukizi ya Ebola

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza rasmi kumalizika kwa maambukizi ya ugonjwa hatari wa Ebola nchini humo.

Maafisa wa afya nchini DRC
Maafisa wa afya nchini DRC congovoice.org
Matangazo ya kibiashara

Waziri wa afya Oly Ilunga ametoa hakikisho hili baada ya kusema kuwa hakuna kisa chochote cha maambukizi mapya yaliyoshuhudiwa ndani ya siku 42.

Ugonjwa wa Ebola uliripotiwa nchini humo  mwezi Mei katika eneo la Kaskazini Mashariki, na kusababisha vifo vya watu wanne na zaidi ya 20 kuambukizwa.

Soma hii pia.Bonyeza hapa.

Shirika la afya duniani WHO limeipongeza serikali ya DRC kwa namna ilivyoshughulikia maambukizi haya na kutoa taarifra za mara kwa mara kwa raia wake.

Ebola iliripotiwa kwa mara ya kwanza nchini DRC mwaka 1976 na kusambaa katika maeneo mengine ya dunia.

Ugonjwa huu bado hauna dawa.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.