Pata taarifa kuu
WFP-NIGERIA-JAMII

WFP: Hatuna fedha za kukidhi mahitaji ya walengwa Nigeria

Shirika la Mpango wa chakula duniani WFP linasema limekabiliwa na uhaba wa fedha, itaweza tu kutoa msaada kwa watu 400,000 waliokimbia makwao Kaskazini mwa Nigeria kutokana na tishio la kundi la kigaidi la Boko Haram.

Wanawake wakipokea chakula kutoka kwa shirika la Mpango wa Chakula Duniani, WFP katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Banki, katika jimbo la Borno, Nigeria, Aprili 26, 2017.
Wanawake wakipokea chakula kutoka kwa shirika la Mpango wa Chakula Duniani, WFP katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Banki, katika jimbo la Borno, Nigeria, Aprili 26, 2017. REUTERS/Afolabi Sotunde
Matangazo ya kibiashara

WFP inasema ilikuwa imepanga kuwafikia watu Milioni 1 nukta 8 mwaka huu lakini ukosefu wa fedha umewalazimisha kubadilisha mipango yao.

Umoja wa Mataifa unasema unahitaji Dola za Marekani Bilioni 1.05 kuwasaidia watu hao.

Wakati huo huo wapiganaji wa Boko Haram wamefanya mashambilizi makali katika mji ulioko kaskazini mashariki mwa Nigeria.

Watu walioshuhudia wanasema mashambulizi hayo makali yametokea wakati waislamu wakijiandaa kufuturu katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Picha ya video ambayo haijathibitishwa iliyotumwa katika mtandao wa Twitter inaonesha wanawake na watoto wakikimbia kutokana na mashambulizi hayo.

 

Wapiganaji wa Boko Haram wameteketeza eneo la kaskazini mashariki mwa Nigeria kwa kuua maelfu ya watu na kulazimisha wengine milioni mbili kuyakimbia makaazi yao.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.