Mali yamtaka raisi Jammeh kuondoka madarakani
Raisi wa Mali Ibrahim Boubacar Keita ametoa wito wa kumtaka kiongozi wa Gambia Yahya Jammeh kuondoka madarakani mara muda wake utakapokoma ili kuepusha taifa kuingia katika umwagaji damu na kulazimisha uvamizi wa kijeshi.
Imechapishwa:
Mzozo wa Gambia ulitawala majadiliano katika mkutano ulioandaliwa na ufaransa nchini Mali,ambapo raisi Mteule wa Gambia Adama Barrow alifika kwa kushtukiza na kukutana na viongozi wa Afrika magharibi kutaka usaidizi wa kumaliza mvutano uliopo.
Raisi wa Mali Ibrahim Boubacar Keita aliwaambia wanahabari kuwa mnamo januari 19 nataraji kuona busara za kiafrika zikimshawishi ndugu Jammeh ambaye ni muislamu mwema kuelewa hatima ya Gambia haihiaji umwagaji damu.
Barrow anataraji kuapishwa mnamo January 19 mara utawala wa raisi Jammeh unapofikia ukomo,ingawa kiongozi huyo amekataa kukabidhi madaraka akidai kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi Barrow.