Pata taarifa kuu
MALI-ANSAR DINE

Kiongozi wa Ansar Dine atangaza kusitisha vita

Kiongozi wa waasi wa kundi la Ansar Dine nchini Mali, amekubali kukomesha mashambulizi kaskazini mwa nchi hiyo yaliyosababisha vifo vya raia wa kawaida, wanajeshi wa serikali na wale wa Umoja wa Mataifa.

Kundi la Kiislamu la Ansar Dine na kiongozi wake Iyad Ag Ghaly, kwenye safa ya kwanza, wakiswali, Machi 11, 2011.
Kundi la Kiislamu la Ansar Dine na kiongozi wake Iyad Ag Ghaly, kwenye safa ya kwanza, wakiswali, Machi 11, 2011. Reuters / Ansar Dine
Matangazo ya kibiashara

Kundi la Ansar Dine ambalo limekuwa likishirikiana na kundi la Al Qaeda, limekuwa likitekeleza mashambulizi kaskazini mwa Mali tangu mwaka 2012, kabla ya kuonekana kuelemewa na wanajeshi wa Ufaransa.

Mwandishi wa RFI mjini Bamako nchini Mali Serge Daniel amesema kuwa mwenyekiti wa Baraza la kitaifa la Waisilamu nchini Mali, Mahamoud Dicko, ameliambia shirika la habari la Uingereza la Reuters kuwa, kiongozi wa Ansar Dine, Iyad Ag Ghali, anatarajiwa kuifamisha serikali ya Bamako.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.