Pata taarifa kuu
ZIMBABWE-MAANDAMANO

Mvutano nchini Zimbabwe: Mgomo mpya Jumatano hii

Nchini Zimbabwe, mvutano unaendelea kushuhudiwa wakati ambapo mgomo mpya unatarajiwa kufanyika Jumatano hii katika mji mkuu, Harare. Vyama vya kiraia vimewataka wananchi wa Zimbabwe kubakia nyumbani katika maandamano dhidi ya serikali ya Rais Robert Mugabe.

Harare, wakati wa mgomo ilikupinga namna nchi ya Zimbabwe inavyotawaliwa, tarehe 6 Julai 2016. Hapa katika eneo la bishara katikati mwa mji mkuu wa Zimbabwe, ambalo liko patupu kutokana na mgomo.
Harare, wakati wa mgomo ilikupinga namna nchi ya Zimbabwe inavyotawaliwa, tarehe 6 Julai 2016. Hapa katika eneo la bishara katikati mwa mji mkuu wa Zimbabwe, ambalo liko patupu kutokana na mgomo. REUTERS/Philimon Bulawayo
Matangazo ya kibiashara

Ni miezi kadhaa sasa maandamnao yakiendelea kushuhudiwa nchini humo.

Mashirika yote ya kiraia nchini Zimbabwe yamewataka raia kusalia makwao. "Wazimbabwe hawawezi tena," alisema Mchungaji Evan Mawarire, mmoj awa waandaaji wa mgomo huo. Ni lazima kutuma ujumbe kwa serikali, ameongeza, Mchungaji Mawarire, katika videoiliyorushwa kwenye mitandao ya kijamii.

"Serikali hii inaendelea kutupiga, kutuweka jela, wakati ambapo hakuna kosa tunalofanya, tunaandamana kwa amani. Tunaheshimu sheria, kwa hiyo Serikali iache kuivunja kwa kutushambulia. Pia, Wazimbabwe, tunawatolea wito wa kudumisha umoja. Serikali hii inapaswa kuelewa kwamba tumechoka kwa namna tunavyohudumiwa. Tuna mawazo ya kuendeleza nchi hii, lakini hawataki kutusikiliza. "

Wote wanadai kujiuzulu kwa Robert Mugabe, ambaye yuko madarakani kwa miaka 36 sasa, na wanamshtumu kwamba anahusika kwa kuanguka kwa uchumi wa nchi. Kiwango cha ukosefu wa ajira kinakadiriwa kuwa zaidi ya 80% na nchi, hata hivyo, nchini sarafu za kitaifa na inakabiliwa na mfumuko wa bei.

Vuguvugu la Tajamuka, ikimaanisha "Tunahangaika," limeahidikuingia mitaani kila wiki hadi kuondoka kwa Rais Robert Mugabe.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.