Serikali nchini Tanzania imefuta usajili wa baadhi ya Vituo vya tiba asilia,na vingine kusitisha huduma zao kutokana na kukiuka masharti ikiwemo urushaji wa matangazo yasiyokuwa na kibali kutoka katika baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala pamoja na baadhi ya waganga kuendelea kutoa elimu ya tiba asili na tiba mbadala kwa umma kinyume cha katazo la wizara ya afya.hivi karibuni kumekuwepo na baadhi ya matangazo na vipindi vinavyorushwa katika redio, magazeti, runinga na mitandao ya kijamii kuhusu utoaji wa matibabu ya tiba asili na tiba mbadala kinyume cha utaratibu na maadili.
Vipindi vingine
-
09:41
-
Mgombea wa upinzani Bassirou Diomaye Faye mwenye umri wa miaka 44 ashinda uchaguzi nchini Senegal
27/03/202409:48 -
Mgomo wa madaktari nchini Kenya, na sekta ya afya katika mataifa ya Afrika.
Kwa karibu wiki mbili sasa, madaktari nchini Kenya wamekuwa kwenye mgomo kulalamikia mazingira ya kazi na kushinikiza kuajiriwa kwa madaktari zaidi.Hali kama hii ya mgomo pia ikishuhudiwa katika miezi ya hivi karibuni nchini Nigeria.Hali katika sekta ya afya nchini mwako ikoje?Serikali za Afrika zifanye nini kuepusha migomo kwenye sekta ya afya?26/03/202409:57 -
09:31
-
Hatua ya Gambia kuondoa marufuku ya ukeketaji wa wanawake na wasichana
Mamia ya raia wa Gambia wakiwemo wanawake wamefanya maandamano juma hili kuunga mkono sheria inayohalalisha ukeketaji wa wasichana na wanawake20/03/202410:08