Pata taarifa kuu
TANZANIA-MAENDELEO-UCHUMI

Tanzania yanyimwa dola 472 kufuatia uchaguzi Zanzibar

Shirika la Marekani linalohusika na malengo ya Milenia limesema limesitisha msaada wake wa Dola Milioni 472 kwa serikali ya Tanzania, kutokana na marudio ya uchaguzi Visiwani Zanzibar.

Wafuasi wa upinzani walikusanyika nje ya makao makuu ya CUF Zanzibar tarehe 28 Oktoba, baada ya kutangazwa kuwa uchaguzi umefutwa.
Wafuasi wa upinzani walikusanyika nje ya makao makuu ya CUF Zanzibar tarehe 28 Oktoba, baada ya kutangazwa kuwa uchaguzi umefutwa. AFP PHOTO / TONY KARUMBA
Matangazo ya kibiashara

Fedha hizo zilinuiwa kuisadia serikali ya Tanzania kuunganisha umeme kwa raia wake wa vijijini.

Waziri wa Mambo ya nje wa Tanznaia Augustine Mahiga amesema ameshangazwa na hatua hiyo na kusema shirika hilo halikuzingatia juhudi za demokrasia zilizopigwa nchini Tanzania.

Marekani na Mataifa ya Ulaya, yalipinga kufanyika kwa marudio ya uchaguzi uliosusiwa na chama kikuu cha upinzani CUF kwa kile ilichosema kuwa uchaguzi wa mwaka jana ulikuwa huru na halali.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.